Tuesday 8 May 2018

MAGUFULI AMGOMEA GEKUL

 Rais John Magufuli amesema hawezi kuingia mgogoro wa Halmashauri ya Babati Mkoani Manyara inayoongozwa na Chadema kulalamikia kunyang'anywa stend na CCM.

Rais Magufuli aliyasema hayo kwenye eneo la Bicha Wilayani Kondoa mkoani Dodoma wakati akizinduzi barabara ya lami ya Babati-Dodoma yenye urefu wa kilometa 251.

Alizungumza hilo mara baada ya mbunge wa jimbo la Babati Mkoani Manyara Paulina Gekul (Chadema) kumuomba Rais Magufuli aagize CCM iwarudishie stendi iliyokuwa inaingiza mapato ya halmashauri ya mji wa Babati. 
 Rais John Magufuli amesema hawezi kuingia mgogoro wa Halmashauri ya Babati Mkoani Manyara inayoongozwa na Chadema kulalamikia kunyang'anywa stend na CCM.

Rais Magufuli aliyasema hayo kwenye eneo la Bicha Wilayani Kondoa mkoani Dodoma wakati akizinduzi barabara ya lami ya Babati-Dodoma yenye urefu wa kilometa 251.

Alizungumza hilo mara baada ya mbunge wa jimbo la Babati Mkoani Manyara Paulina Gekul (Chadema) kumuomba Rais Magufuli aagize CCM iwarudishie stendi iliyokuwa inaingiza mapato ya halmashauri ya mji wa Babati. 
Aliwataka wananchi wa mikoa inayopita barabara hiyo waitunze ili iweze kudumu kwa miaka mingi zaidi na kuwanufaisha kiuchumi.

Alimpongeza Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete kwa kuweka jiwe la msingi barabara hiyo wakati Rais Magufuli akiwa Waziri wa ujenzi.

"Nakumbuka wakati huo wabunge wa eneo hili Nkamia na mama Zabien Mhita ambao niliwaomba waniunge mkono kwa kupisha bajeti ili barabara ijengwe," alisema Rais Magufuli.

Waziri wa Ujenzi Profesa Makame Mbarawa alisema barabara hiyo ni miongoni mwa eneo la barabara kuu ya kaskazini yenye kilomita 10, 228 kutoka jiji la Cape Town nchini Afrika kusini hadi jijini Cairo nchini Misri.

Waziri Mbarawa alisema barabara hiyo imegharimu kiasi cha sh378 bilioni, ambapo serikali ya Tanzania imetoa sh107 bilioni, benki ya maendeleo ya Afrika (ADB) sh203 bilioni na shirika la maendeleo la Japan (Jica) sh67 bilioni.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti akizungumza kwenye uzinduzi huo alisema awali wananchi wa eneo hilo walikuwa wanatumia siku nzima kusafiri kati ya Babati hadi Dodoma ila hivi sasa wanaotumia muda wa saa mbili.

"Hivi sasa mtu anaweza kwenda Dodoma na kurudi Babati hata mara tatu na pia anaweza kutumia usafiri wa bajaji kwa kutumia barabara hii," alisema Mnyeti.

Alimpongeza Rais Magufuli kwa namna anavyoongoza nchi  na kusababisha wao wasaidizi wake kufuata nyayo zake kwa kufanya kazi kwa bidii.

Mtendaji mkuu wa wakala wa barabara nchini (Tanroads) mhandisi Patrick Mfugale alisema mradi wa barabara ya Dodoma-Babati umegharimu kiasi cha sh378 bilioni.

Mhandisi Mfugale alisema barabara hiyo ambayo imeunganishwa na barabara kuu ya kutoka Afrika kusini hadi Misri, itadumu kwa muda wa miaka 20 na madaraja yatadumu kwa miaka 120.

Balozi wa Japan Masaharu Yoshida alisema kwa kushirikiana na benki ya maendeleo ya Afrika (ADB) wamewezesha kufanikisha ujenzi wa barabara mbili nchini ambazo zote zimekamilika.

Balozi Yoshida alisema mradi mwingine ni ujenzi wa barabara ya Tunduru, Mangaka hadi Mtambaaswala, ambayo nayo imekamilika.

Alisema mradi wa barabara hiyo ulikamilika Octoba 2017  na ulizinduliwa na Rais Magufuli Aprili 27 mwaka huu.

Rais wa benki ya maendeleo ya Afrika, (ADB) Dk Akinwumi Adesina alisema jamii za vijijini zitakuwa na manufaa makubwa ya kiuchumi kupitia barabara hiyo.


Dk Adesina alisema wasafiri na wafanyabiashara nao watanufaika na biashara mbalimbali kwa kutumia barabara hiyo ambayo itatumika kunyanyua uchumi wao.

No comments:

Post a Comment