Thursday 25 August 2016

WAJUMBE WA STAMICO WATEMBELEA MIGODI YA TANZANITEONE



Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la madini nchini (STAMICO) wakiwa na baadhi ya watumishi wa kampuni ya TanzaniteOne na STAMICO walipotembelea mgodi wanaoumiliki kwa ubia na kampuni hiyo uliopo mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.



Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la madini nchini (STAMICO) Zena Kongoi akizungumza na waandishi wa habari,  kwenye mgodi wa kampuni ya TanzaniteOne.

 Zena Kongoi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la madini nchini (STAMICO) akizungumza na waandishi wa habari.


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la madini nchini (STAMICO) Zena Kongoi akizungumza kwenye migodi ya Tanzanite.


Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya TanzaniteOne, Robert Grafen.


Wajumbe wa bodi ya STAMICO wakiwa na Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Balozi Alexiander Muganda, (wa pili kushoto) baada ya kutembelea mgodi wanaoumiki kwa ubia na kampuni ya TanzaniteOne uliopo mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.



Wajumbe bodi ya STAMICO wakipanda scip kwa ajili ya kuingia kwenye mgodi wa madini ya Tanzanite uitwao CT.