Monday 28 April 2014

MAGAZETI LEO JUMANNE 29 APRILI 2014

.
.
Ni utaratibu wa millardayo.com kila siku kukupa nafasi ya kusoma kurasa za mwanzo na mwisho za magazeti mbalimbali ya Tanzania.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

UZINDUZI, HARAMBE NA KIPAIMARA BABATI


Askofu wa Jimbo la Mbulu Mkoani Manyara, Beatus Kinyaiya akiweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa kanisa jipya la Parokia ya Roho Mtakatifu mjini Babati, linalotarajia kugharimu sh915 milioni, ambapo aliwapa kipaimara vijana 116 na kuendesha harambee na shilingi 28,322,000 zilipatikana jumapili iliyopita.

Miongoni mwa vijana 116 waliopewa kipaimara na Askofu wa Jimbo la Mbulu Mkoani Manyara, Beatus Kinyaiya jumapili iliyopita kwenye kanisa la Parokia ya Roho Mtakatifu mjini Babati.

Umati wa watu waliohudhuria kwenye kanisa Katoliki Parokia ya Roho Mtakatifu Dikonia ya Babati Mkoani Manyara, ambapo Askofu wa Jimbo la Mbulu, Beatus Kinyaiya aliwapa kipaimara vijana 116, aliweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa kanisa jipya la Parokia ya Roho Mtakatifu, linalotarajia kugharimu sh915 milioni na akaendesha harambee iliyokusanya shilingi 28,322,000.

BEI YA TANZANITE YAPANDA NCHINI



Na Mussa Juma, Mwananchi

Arusha.Bei ya madini ya Tanzanite yanayopatikana kwenye machimbo ya mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, hapa nchini imepanda huku bei hiyo ikiporomoka katika soko la kimataifa.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kwa wafanyabiashara kadhaa wa madini na wachimbaji wa madini hayo, umebaini kupanda kwa bei ya madini hayo hapa nchini, kunatokana na uzalishaji kupungua migodini.

Kwa sasa bei hiyo, imepanda kati ya Sh100,000 hadi Sh500,000 kwa gramu moja ya Tanzanite kutokana na ubora na ukubwa.

Hata hivyo, katika soko la kimataifa, bei hiyo imeporomoka kutokana na madini hayo kusafirishwa nje kwa wingi zaidi miaka ya karibuni.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Maruti Green Gems Limited, Faisal Juma Shahbhai, alisema bei ya madini haya imekuwa ikipanda hapa nchini kutokana na uzalishaji kupungua.

Hata hivyo, alisema hali ya utulivu na amani, katika migodi ya Tanzanite pia imechangia kuimarika kwa biashara ya madini hayo hapa nchini.

Mwenyekiti wa Chama cha Wauzaji wa madini  nchini (Tamida), Sammy Mollel alisema kwa sasa uzalishaji wa madini hayo umekuwa mdogo, kutokana na gharama kubwa na uchimbaji.

MWISHO.