Tuesday 20 December 2016

VODACOM YATOA MSAADA KITUO CHA WAZEE SARAME MAGUGU BABATI MANYARA



Meneja ruzuku na mawasiliano wa Vodacom Tanzania Foundation, Sandra Oswald, akimkabidhi, mmoja kati ya wazee wa kituo cha wazee na wasiojiweza Sarame Magugu, Wilayani Babati Mkoani Manyara, Maalim Masaja chandarua, ambapo waliwakabidhi wazee hao mashuka, vyandarua, vyakula, dawa na mahitaji mengine yenye thamani ya zaidi ya sh10 milioni.
Meneja ruzuku na mawasiliano wa Vodacom Tanzania Foundation, Sandra Oswald, akimkabidhi Khadija Omari, mmoja kati ya wazee wa kituo cha wazee na wasiojiweza Sarame Magugu, Wilayani Babati Mkoani Manyara, shuka na vyandarua, baada ya kukabidhi msaada wa vyakula, dawa na mahitaji mengine yenye thamani ya zaidi ya sh10 milioni.

TUZO UTUNZAJI MAZINGIRA

 
Mkuu wa Babati ya Babati Raymond Mushi akiwa ameshika tuzo ya utunzaji mazingira aliyokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dk Joel Bendera
 
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dk Joel Bendera akiwa amemkabidhi Katibu Tawala wa Mkoa huo Eliakim Maswi tuzo ya utunzaji mazingira

Saturday 17 December 2016

WATAKIWA KUONDOA MIGOGORO MANYARA

 Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dk Joel Bendera amewataka viongozi wa Wilaya kuhakikisha wanashirikiana ipasavyo ili kutatua migogoro ya ardhi inayorudisha nyuma maendeleo kwani robo tatu ya mkoa huo imegubikwa na migogoro.
 
Dk Bendera akizungumza mjini Babati kwenye mafunzo elekekezi kwa viongozi wa wilaya za mkoa huo alisema, migogoro ya ardhi kwa kiasi kikubwa ndiyo kikwazo cha maendeleo hivyo watumie uwezo wao wote ili kuimaliza.
 

Alisema kila kiongozi kwa nafasi yake anapaswa kuhakikisha anasimama vyema katika kutekeleza majukumu zaidi kwani migogoro mingi inaweza kumalizika endapo itatiliwa maanani kwenye utekelezaji ili kupiga hatua ya maendeleo.
 
Alisema migogoro ya ardhi ambayo imetawala kwenye robo ya sehemu ya Manyara inapaswa kumalizika kwa kuhakikisha viongozi wote wa wilaya wanawajibika kumaliza migogoro hiyo isiyokuwa na faida yoyote.
 
“Tunapaswa kutimiza wajibu wetu ipasavyo kwa kuhakikisha viongozi wa kisiasa na watendaji wanatumia nafasi zao kikamilifu ili kumaliza migogoro hiyo ambayo haina manufaa kwa wananchi tunaowaongoza,” alisema Dk Bendera.
 


Mkuu wa wilaya ya Kiteto Tumaini Magessa, alisema matatizo mengi ya mkoa wa Manyara kuhusu migogoro hiyo ni kutokuwepo kwa matumizi bora ya ardhi kwani wilaya hiyo imetumia miaka 10 kusuluhisha migogoro na haijamalizika.
 
“Wilaya yetu imetumia miaka mingi mno kwa ajili ya kusuluhisha migogoro ili hali tungeweza kutumia muda huo kwa ajili ya kujenga madarasa, shule na kufanya maendeleo mengine hivyo tunapaswa kubadilika,” alisema Magessa.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Simanjiro Yefred Mnyenzi alisema inapaswa sheria, taratibu na kanuni (STK) zifuatwe katika utekelezaji kwani kuna baadhi ya watu wanamilikishwa ardhi bila kufuata utaratibu halali.
 
Mkuu wa wilaya ya Simanjiro Zephania Chaula alisema viongozi wa wilaya yake na wilaya ya Kiteto watakutana hivi karibuni ili kusuluhisha mgogoro wa ardhi uliopo kwenye kata ya Emboreet Simanjiro na kata ya Makame Kiteto.  
 
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Tamimu Kambona alisema wanakabiliwa na migogoro mingi ya mipaka kwenye wilaya jirani ikiwemo Kilindi, Gairo, Chemba na Simanjiro hivyo mkoa ushiriki kuitatua.