Thursday 29 November 2012

MAHAFALI

Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara,Christopher Ole Sendeka akimkabidhi cheti mmoja kati ya wanafunzi waliohitimu darasa la saba kwenye shule ya msingi Oloshonyokie Kijiji cha Naisinyai.

Sunday 25 November 2012

UZINDUZI UJENZI STAND BABATI

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Babati Mkoani Manyara,Mohamed Omary Farah,akizungumza jana kwenye uzinduzi wa ujenzi wa kituo cha mabasi ya mji huo ambao utajengwa kwa msaada wa kampuni ya kichina ya Chico kwa gharama ya sh50 milioni (kulia) ni Msemaji wa kampuni hiyo Yan Wangting na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa mji huo Winnie Kijazi.

MAJI GALAPO KASHESHE

TATIZO la muda mrefu la uhaba wa maji kwa wakazi wa kijiji cha Galapo Wilayani Babati Mkoani Manyara limesababisha kuvunjika kwa mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Waziri wa maji Profesa Jumanne Maghembe baada ya waziri huyo kuwakejeli wapinzani kuwa hawawezi kuwapa maji wananchi hao.

Hali hiyo ilijitokeza juzi kijijini hapo ambapo Prof Magembe alifika eneo hilo na kutegemewa na wananchi kuwa atavunja Mamlaka ya maji safi na maji taka Galapo (Gawasa) wanaodaiwa kuchukua fedha lakini hawatoi huduma ya maji.

Awali,waziri huyo alizungumza na wakazi hao na kudai kuwa ni lazima wananchi wachangie huduma ya maji ili mamlaka ziweze kununua vifaa vinavyohitajika katika kuendesha miradi husika,kwani hiyo ndiyo sera ya Serikali ya CCM.

“Naagiza kuwa maji yatalipiwa ili huduma iwe endelevu na agizo hili pia nalielekeza kwa mamlaka za maji za miji midogo yote nchini iwe Galapo,Dareda,Magugu na Bashnet,” alisema Prof Maghembe.

Hali ya mkutano huo,ilibadilika baada ya waziri huyo kudai kuwa wapinzani wanakuwa na maneno mengi lakini ukiwaambia watekeleze jambo lolote wana shindwa na kubaki kuilaumu CCM.

“Hawa wapinzani kama ni matusi wacha wanitukane tu lakini suala la kuwapa maji eneo hili hawawezi ni kelele tu za bure nyie endeleeni kuchangia maji mnayotumia kwani ndiyo sera yetu,” alisema Prof Maghembe. 

Kauli hiyo iliamsha nyongo za wakazi hao zilizolala,kwani baadhi yao walianza kuonyesha vidole viwili hewani na kudai kuwa wapinzani wataweza  kuleta maji kwani kuna baadhi ya maeneo wameweza.

Baadhi yao walipasa sauti na kudai kuwa Chadema ina uwezo wa kuleta maji kwani mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki,Joshua Nassari aliweza kuwachimbia maji wakazi wa Maroroni kwa siku tatu wakati CCM ilishindwa kwa miaka 50.

“Mnashindwa kuiondoa Gawasa ambayo inachukua pesa zetu bure za maji lakini huduma yenyewe hawatoi maji unapata kwa wiki mara moja ankara inakuwa ya juu tutaweza wapi maisha haya,” walisema wakazi hao.

Mkutano huo ilivunjika huku Katibu mwenezi wa CCM Babati,Adam Ipingika akiwataka wananchi wakaulize maswali yao Chadema na waziri huyo akaondoka na msafara wake akisindikizwa na kelele na kuonyeshwa vidole viwili na baadhi ya wakazi hao.

MWISHO.

Thursday 22 November 2012

WAANDISHI WA HABARI

Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Manyara kutoka kushoto,Fortunatha Ringo,Joseph  Lyimo,Julieth Peter na Mary Margwe wakiwa mji mdogo wa Galapo Wilayani Babati kwenye ziara ya Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe.

Tuesday 20 November 2012

JK AKIHANI MSIBA WA MAKWETA

RAIS JAKAYA KIKWETE AKITIA SAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO CHA MAREHEMU JACKSON MAKWETA

Saturday 3 November 2012

JK NA DIWANI WA ENDIAMTU

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Diwani wa Kata ya Endiamtu Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara Lucas Zacharia baada ya kuwasili eneo la Sinai mjini Babati kwenye ziara ya siku mbili mkoani humo kwa ajili ya kuzindua na kukagua miradi ya barabara,maji na kukagua shughuli za wajasiriamali