Monday 31 July 2017

MHESHIMIWA ANNA GIDARRYA:HATUTETEI WEZI MALI ZA UMMA TUNAKWEPA KUENDELEA KUACHIWA MAGOFU KWENYE MACHIMBO YA MADINI


ASEMA WANAOSEMA UPINZANI WANATETEA WEZI NI SIASA ZA MAJI TAKA. 

Wananchi wametakiwa kupuuza habari mbalimbali za kizushi zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ambazo zinaeleza kuwa vyama vya upinzani vinapinga juhudi za maendeleo na kutetea wezi wa mali za umma wakiwemo mafisadi.

Kauli hiyo ameitoa Mbunge wa viti maalum wa Mkoa wa Manyara Anna Gidarya akizungumza kwenye uzinduzi wa albamu ya kwaya ya Ukombozi ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) na umati na Usharika wa Haydom Mtaa wa Bethania. 

“Kuna watu wamekuwa wasemaji wakuu kwenye mitandao ya kijamii huwenda nyie watu wa Bethania hamuingii sana kwenye mitandao kulingana na mazingira ya huku watu wanasema wapinzani wamekuwa wakimpinga Rais John Magufuli hatupingi juhudi zozote za rais tunachotaka upinzani hatutaki kurejea miaka 54 iliyopita kuingia katika mikataba mibovu inayopelekea nchi yetu kutofaidika na rasilimali zilizopo wawekezaji wamekuja wamechimba madini yetu wametuachia mashimo hatutaki kuendelea kuwa hivyo tuanataka mambo yaende sawa sawia na si kupinga maendeleo yoyote ya nchi,” alisema Gidarya.

Aliwataka wananchi wilayani mbulu na mkoa mzima wa Manyara kutokukubali kuendelea kutokuamini habari za mitandao ya kijamii zinzozushwa ikiwemo kile alichoeleza kuwa habari zenye udini ili kuepeuka kuliingiza taifa katika uvunjifu wa amani na umoja wa  Taifa.

“Ndugu zangu kuna watu wengine wanasmabaza habari ambazo zina udini nawaombeni tusifanye siasa kwenye mioyo ya waliowengi na tutaishia pabaya manona yanayoendelea kibiti kuna watu wanahusisha na udini hatuna uhakika nawaombeni ndugu zangu habari za namna hii kwamba kuna kiongozi anazungumzia masuala ya udini naombeni mzipuuze ni siasa chafu ambazo hazina ishara nzuri kwa taifa letu,” alisema Gidarya.

Kwa upande mwingine Mmbunge huyo ameiasa jamii  hususan wananchi wa mkoa wa Manyara kuhifadhi chakula kilichopatikana kutokana na hali mbaya ya hewa ili kuodnokana na kukumbwa na baa la njaa siku zo usoni.
“Kina mama uzuri hapa leo hatuzungumzi kwenye majukwaa na hapa tunazungumza na watu wanao mjua Mungu watu wa bethania kila mmoja anajua Mama mzuri na baba mzuri kila awae mzazi mnajua mzazi mzuri ni Yule anayekumbuka kuhifadhi akiba ya chakula kwaajili ya familia yake hifadhini chakula serikali haina hata maghala haina chakula cha akiba kugawa kwa wananchi wake itakapotokea njaa,” mheshimiwa Anna Gidarya alisema.

Mheshimiwa Anna pia amewahimiza akina mama na vijana kufika katika ofisi za halmashauri zao kuuliza juu ya utaratibu wa asilimia hamsini ambazo zinatengwa kwaajili ya kugawiwa vikundi vya vijana na akina mama kwaajili ya kuanzisha miradi ya kujiendeleza kiuchumi.

“Nendeni kwenye hamalshauri ulizeni hiyo asilimia ni haki yenu mfuateni diwani muulizeni pia juu ya fedha hizo awape ufafanuzi hizo fedha zipo kwa ajili ya vikundi vyenu,” alisema Gidarya.

Naye muinjilisti kiongozi wa kanisa la Bethania usharika huo wa hydom ameungana na Mmbunge huyo kwa kumshukuru kwa dhati kwa kutoa elimu hiyo na hamasa hiyo kwa vikundi kwa vijana na akina mama kwani ni jambo muhimu sana jamii kukumbushwa juu masuala hayo.

“Mheshimiwa mbunge mi niseme tu nimefurahishwa na elimu ulioitoa leo hapa kwa waumini na wananchi hawa unajua ni bora mtu akupe elimu kuliko akupe fedha jamani ndugu zangu nimefurahishwa leo na mheshimiwa Mmbunge kutoa elimu hii bora mtu akupe elimu kuliko akupe kitu kingine tukushukuru sana Mheshimiwa Mmbunge mungu akubariki” Petro Emmanuel alisema.

Katika uzinduzi wa albamu hiyo ya kisulisuli ya kwaya ya ukombozi iliyobeba myimbo kumi Mheshimiwa Mmbunge Anna Gidarrya ameweza kuchangia zaidi ya milioni sita katika kuchangia kwa hiyo kuweza kuendelea na kazi yake ya kutangaza injili kupitia nyimbo za injili.




No comments:

Post a Comment