Friday 23 February 2018

WAKUU WA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA WATEMBELEA UKUTA MIRERANI



Mkuu wa majeshi ya ulinzi ya wananchi Tanzania, Venance Mabeyo (kushoto) akionyeshwa ramani na Mkurugenzi mwendeshaji wa Suma JKT ujenzi, mhandisi Morgan Nyonyi, ya ukuta uliojengwa kuzunguka migodi ya madini ya Tanzanite ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, alipotembelea eneo hilo jana, katikati ni mkuu wa polisi nchini, IGP Simon Sirro.



Wakuu wa vyombo vya ulinzi, usalama, magereza na uhamiaji nchini, wakiwa kwenye lango la ukuta uliojengwa kuzunguka migodi ya madini ya Tanzanite yaliyopo Mji mdogo wa Mirerani.



Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Simon Sirro, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea eneo lililojengwa ukuta katika machimbo ya madini ya Tanzanite, Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara.

Wakuu wa vyombo vya ulinzi, usalama, magereza na uhamiaji nchini, wakiwa kwenye lango la ukuta uliojengwa kuzunguka migodi ya madini ya Tanzanite yaliyopo Mji mdogo wa Mirerani.


Mkurugenzi mwendeshaji wa Suma JKT ujenzi, mhandisi Morgan Nyonyi, akionyesha ramani ya ukuta uliojengwa kuzunguka migodi ya madini ya Tanzanite ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kwa viongozi wa kitaifa wa kamati ya ulinzi, usalama, magereza na uhamiaji walipotembelea eneo hilo.





No comments:

Post a Comment