Monday 12 May 2014

SIKU YA WAUGUZI


Rais Jakaya Kikwete akisikiliza maelezo ya namna wauguzi wanavyotoa huduma zao kwenye maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani iliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini Arusha .


Rais Jakaya Kikwete ametoa wito kwa wananchi  kujitaidi kupima afya zao kwanza ili kubaini wanaugua ugonjwa gani kabla ya kutumia dawa.

Rais Kikwete aliyasema hayo wakati alipokuwa akihutubia katika kilele cha sherehe za maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani ambapo kitaifa yalifanyika jana jijini Arusha.

Alisema kuwa ni wajibu wa kila mwananchi kupima afya yake kabla ya kunywa dawa kwani itamsaidia kujua nini  au ugonjwa gani unamsumbaua
Aidha Kikwete akiongelea ugonjwa wa denguae alisema kuwa ugonjwa huu uliongia hapa nchi ni  hatari hivyo ni wajibu wa kila mtanzani anahakikisha ana uthibiti ugonjwa huu.

alisema kuwa  iwapo kila mtu atafuata mashariti ikiwa ni pamoja na kulala ndani ya chandalua chenye dawa ,pamoja na kufukia madibwi yote basi ugonjwa huu unaweza kutoweka kabisa .



kwa upande wa wauguzi alisema kuwa amesikia kero zao na atazifanyia kazi kwa yale ambayo yatawezekana, badhi ya matatizo ya wauguzi ambayo wameyataja mbele ya  Rais ni pamoja na kuitaji malipo ya mazingira hatarishi, walitaka vyeo vipandishwa kwa wakati pamoja na kulipwa malipo ya likizo kwa wakati. 

Pia waliomba ruzuku kwa masomo ya juu pamoja na kuboreshewa maeneo ya kazi.

No comments:

Post a Comment