Monday 12 May 2014

MISS MANYARA KUTIMUA VUMBI MEI 31 MWAKA HUU

 Miss Redds Photogenic 2012 Lucy Stephano kutoka kwenye Kijiji cha Ngwandwakw, Kata ya Haydom Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara.

Mashindano ya kumsaka mrembo wa Mkoa wa Manyara, Miss Manyara 2014 inatarajia kufanyika mjini Babati May 31 mwaka huu ambapo washiriki 15 wa kutoka Wilaya za Simanjiro, Hanang’ Mbulu, Kiteto na Babati wanatarajia kushiriki.

Mratibu wa kampuni ya Mirerani Entertainment ya mjini Babati, Akon Clement, ambao ndiyo waandaaji wa mashindano hayokizungumza na waandishi wa habari juzi alisema maandalizi ya mashindano hayo yanaendelea vizuri.

'Hivi sasa maandalizi ya kufanyika kwa Miss Manyara, yanaendelea vizuri kwani washiriki kutoka kwenye wilaya hizo wanaendelea na mazoezi kwa ajili ya kupatikana kwa wawakilishi wa mkoa huo," alisema Clement.

Alisema wapo kwenye mazungumzo na baadhi ya waadhamini waliotuahidi kutuunga mkono kwenye Missi Manyara 2014, kwani mdhamini mkuu ni kampuni ya Tanzania Breweries kupitia kinywaji chake cha Redds.

Alitaja baadhi ya wadhamini wanaotarajia kudhamini Miss Manyara 2014 ni Manyara Compyuta, Chuo kikuu huria Manyara, Motel Silver, Trimas Saloon, Mireranitanzanite.blogspot.com, Shambani Solution Green belt na Fear Deal.

“Wadhamini wengine wanaotarajia kutudhamini kwenye shindano letu ni Motel Silver, Tina Classic, Pole pole Coach, San Abima Classic, Alno Technology, Ziggy Supermarket na Code Marketing,” alisema Clement.

Alitoa ombi kwa wazazi na walezi wa wilaya za mkoa huo, kuwapa ruhusa mabinti wao ili waweze kushiriki mashindano hayo, kwani mabinti wa jamii za wairaqw, wadatoga, wamasai, wambugwe na wafyomi wana uzuri wa asili.

“Pia tunaendelea na mazungumzo na baadhi ya wasanii wakubwa wa muziki kutoka jijini Dar es salaam na wasanii wengine chipukizi wa hapa hapa Babati na mkoa mzima wa Manyara kwa ujumla watashiriki,” alisema Clement.

No comments:

Post a Comment