Tuesday 18 December 2012

KAMANDA SURUMBU

NAIBU Katibu Mkuu wa NCCR Mageuzi,Lawrence Surumbu Tara ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Bashnet Wilayani Babati Mkoani Manyara amejivua uanachama na kujiondoa kwenye chama hicho na kujiunga na Chadema.
Tara ambaye alikuwa diwani wa kata ya Bashnet kwa tiketi ya chama cha NCCR-Mageuzi tangu mwaka 200 hadi Desemba 17,alitangaza uamuzi huo jana mjini Babati mbele ya waandishi wa habari akiwa na Mjumbe wa Kamati kuu ya Chadema Godbess Lema na kiongozi mwingine wa Chadema Ally Bananga.

No comments:

Post a Comment