Tuesday 18 December 2012

KAMANDA TARA

Naibu Katibu Mkuu wa chama cha NCCR-Mageuzi (Bara) Lawrence Surumbu Tara ambaye pia ni Diwani wa kata ya Bashnet Wilayani Babati Mkoani Manyara (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Babati ambapo alitangaza rasmi kujivua udiwani na vyeo vyote alivyokuwa navyo NCCR-Mageuzi na kujiunga na Chadema (kushoto) ni aliyekuwa mbunge wa Arusha Godbess Lema na,Kamanda Ally Bananga.


Alisema yeye ni mmoja wa waathirika wa mfumo huo mbovu wenye dhuluma kwani alidhulumiwa ubunge kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 na kwa bahati mbaya wizi huo wa kura unaongeza maovu.
Alisema yeye alishinda ubunge wa Jimbo la Babati Vijijini kwa kupata kura kura 32,248 na mgombea wa CCM akapata kura 30,190 lakini baadhi ya wasimamizi v wakabadilisha matokeo na kumpa mgombea wa CCM kura 32,777 na yeye 31,635.
“Kule Dareda niliibiwa kura 156 na shule ya msingi Riroda niliibiwa kura 300 na Chadema wakaibiwa kura 10 ambazo zilijumlishwa kwa CCM na akaongezea kura hewa 48 kwenye shule ya msingi Riroda namba 4 na Mwada shule ya msingi shauri moyo CCM walipewa kura hewa 400.
Alisema katika mazingira hayo amebakiwa na chaguo moja wapo kati ya kubaki ndani ya chama kisichokerwa na wizi wa kura na ambao baadhi ya viongozi wake wanaendeleza urafiki na mfumo huo uliokithiri.
“Nikaona kujitenga na kuachana na chama chenye viongozi wa aina hiyo na kutafuta chama imara ambacho hakina simile na mambo kama ya aina hio chenye kupigania haki,ukweli na ambacho kimepania utawala bora na ustawi wa watanzania,” alisema.
na,Kamanda Ally Bananga.


No comments:

Post a Comment