Tuesday 18 December 2012

LAWRENCE

Akizungumza wakati akitoa tamko lake la kujitoa NCCR Mageuzi na kujiunga na Chadema,Tara alisema amejitoa kwenye chama hicho akiwa na sababu kuu mbili zilizosababisha yeye kuhama chama hicho.
Alizitaja sababu hizo kuwa ni baadhi ya viongozi wa NCCR Mageuzi kupendelea au kuendeleza urafiki na mfumo dhalimu wa dhuluma na maovu yanayofanywa na dola chini ya Serikali ya CCM.
Alisema kutokana na hali halisi ya kisiasa nchini ilipofika na kwa jinsi dhuluma na maovu kushamiri nchini kiasi cha kufikia watumishi na viongozi wa umma kudhulumu na kufanya maovu kwa uhuru mkubwa bila hofu ya kuadhibiwa.
“Tunahitajika chama cha siasa,kilicho makini na ambacho watanzania tunapaswa kuunganisha nguvu zetu kwa pamoja bila kutengana na kwa maoni yangu NCCR Mageuzi siyo chama cha aina hiyo,” alisema Tara.

No comments:

Post a Comment