Saturday 9 June 2018

DC MOFUGA AANZISHA KAMPENI YA VYETI KWA MANUFAA YA WANANCHI MBULU

 Dc Mbulu aanzisha kampeni ya vyeti vya kuzaliwa, vifo na ndoa kwa manufa ya wananchi.

Mkuu wa wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara Chelestino Simbalimile Mofuga ameanzisha kampeni ya wananchi wilayani Mbulu ya vyeti vya kuzaliwa, vifo na ndoa.

kampeni hiyo imezinduliwa katika kata tatu ikiwemo kata ya Ayamaami, Uhuru na kata ya Imboru.

Mofuga amesema ni vyema kila mwananchi kuwa na cheti cha kuzaliwa ili kuepuka usumbufu na kutambulika katika eneo lake  kwani mwananchi akiwa na cheti cha kuzaliwa anakuwa salama na akihitaji huduma ni rahisi kuhudumiwa katika eneo lake.

pamoja na hilo amesema vyeti vya ndoa na vifo ni muhimu sana kwa mwananchi ili inapotokea mmoja amefariki itamsaidia ailiyebaki katika kusimamia mirathi bila kuingiliwa na mtu yeyote wa upande mwingine.


Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Mbulu amesema kwamba wilaya ya Mbulu inakabiliwa na  changamoto ya matumizi ya risiti na kuwataka wananchi kutoanunua bidhaa katika maduka ambayo hayatoi risiti ili kuepuka usumbufu wa kupelekwa kwenye vyombo vya sheria kwani mwananchi akikamatwa ana bidhaa aliyonunua bila risiti atafikishwa kwenye vyombo vya sheria.

katika maeneo hayo aliyoyapitia nakufanya mkutano wa hadhara mkuu wa wilaya amewataka wananchi kutopika wala kunywa pombe haramu aina ya gongo na pia kutouza pombe kabla ya saa tisa alasiri.

Kwa kata ya Uhuru ameagiza wenyeviti wa mitaa kusimamia wananchi wasinywe pombe kabla ya saa tisa vinginevyo watawajibika wao wenyewe kwani mtaa wa Uhuru unasifika sana kwa unywaji wa pombe badala ya kufanya kazi.

Katika kata tatu alizoanza nazo tarehe 8.06.2018 katika kata tatu ambazo ni kata ya Ayamaami,uhuru na Imboru kata ya Imboru mahudhurio hayakuwa mazuri na ameagiza wenyeviti wa mitaa siku  ya tarehe 11.06.2018 kufika katika ofisi yake wakiwa na maelezo ya kutosha ya kwanini wananchi hawajajitokeza.

Pamoja na maelezo hayo amewataka wenyeviti waende na tozo ya shilingi 5,000/ kwa kila kichwa kwa wale wote  ambao hawahudhuria kikao chake cha kiserikali yenye lengo la kutoa maagizo muhimu.

Amesema wananchi wote ambao hawajashiriki mkutano wake wanafikia 1004  na kwa tozo hizo watakazotoa watafikisha million tano ambayo imepitishwa kupelekwa kwenye shule ya msingi Isale kwa ajili ya kupeleka maji.

Kauli mbiu cheti cha kuzaliwa nyumba kwa nyumba


No comments:

Post a Comment