Saturday 13 July 2013

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAZURU MIRERANI

                                                                    

Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya kudumu ya Nishati na Madini, Mhe Anne Kilango Malecela (katikati) Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo,Mhe Richard Ndassa (kushoto) na Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kaskazini, Benjamin Mchwampaka wakiwa kwenye mkutano na wachimbaji wadogo wa Madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani.



Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya kudumu ya Nishati na Madini, Mhe Anne Kilango Malecela (katikati) akiongozwa na Mchimbaji wa madini ya Tanzanite (kushoto) Mohamed Karia ambaye ni Mkurugenzi wa kampuni ya Tan Youth Mining Ltd ambayo wachimbaji wadogo wanaiomba Serikali iifutie kodi na iipe kibali cha kuwasambazia zana za milipuko kwa bei nafuu.

                                                                                      

Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, Mhe Christopher Ole Sendeka,akizungumza kwenye kikao cha Kamati ya Bunge ya kudumu ya Nishati na Madini, ilipotembelea wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani.

No comments:

Post a Comment