Friday 21 March 2014

BONDE YAEDA CHINI



Jamii ya wafugaji wa kidatoga wa bonde la Yaeda Chini Wilayani Mbulu Mkoani Manyara, wakiwasikiliza baadhi ya viongozi wa wilaya hiyo waliowatembelea ili kusuluhisha mgogoro wao wa ardhi na jamii ya wairaqw.




Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Christina Mndeme ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Hanang’ akizungumza na jamii ya wafugaji wa kidatoga na wairaqw wa Bonde la Yaeda Chini, ambao wana mgogoro wa muda mrefu,ambapo aliwataka wadumishe amani kwenye eneo hilo.



Mkuu wa polisi wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, SSP George Kyando akizungumza na jamii ya wafugaji wa kidatoga na wairaqw wa Bonde la Yaeda Chini, ambao wana mgogoro wa muda mrefu, ambapo aliwaasa waache vurugu na kutekeleza dhana ya ulinzi shirikishi.




Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Fortunatus Fwema, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Hanang’ akiwaasa jamii ya wafugaji wa kidatoga na wairaqw wa Bonde la Yaeda Chini, ambao wana mgogoro wa muda mrefu kuwa waachane na vurugu na kufanya shughuli zao za kiuchumi za kifugaji na kilimo.

No comments:

Post a Comment