Saturday 8 February 2014

WANA CCM WACHUKUA FOMU KALENGA

Chama Cha Mapinduzi jimboni Kalenga mkoani Iringa kimeanza rasmi mchakato wa kumpata mgombea wa ubunge wa jimbo hilo. Uchaguzi mdogo unatarajiwa kufanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Dk. William Mgimwa.
 
Tayari wanachama tisa wa chama hicho wamekwishachukua fomu kuonesha nia yao ya kuingia katika kinyang'anyiro hicho. Wanachama hao ni Hafsa Mtasiwa, Jackson Kiswaga, Godfrey Mgimwa, Edward Mtakimwa na Thomas Mwakoka.

Wengine ni Gabriel Kalinga, Msafiri Pamagil, Peter Mtisi na Grayson Kibasa.
 
Chama hicho kitaendesha kura ya maoni siku ya Jumamosi tarehe 8 Februari. Kura hiyo ni kwa ajili kupata jina la mgombea mmoja litakalowasilishwa kwenye Tume ya Uchaguzi. 
 
Tume ya Uchaguzi bado haijatangaza rasmi tarehe ya uchaguzi jimboni humo.

No comments:

Post a Comment