Friday 3 October 2014

VURUGU ZA WANAJESHI NA POLISI TARIME/RORYA

Hii ni taarifa kutoka Tarime mkoani Mara ambako watu 12 wamejeruhiwa wakati wa mashambulizi ya kurushiana risasi kati ya askari wa JWTZ kituo cha Nyandoto na polisi wa kituo cha stendi.
 
Kwa mujibu wa magazeti ya Nipashe na Mwanachi leo, hii ishu ilitokea wakati Wanajeshi hao walipokua wakijaribu kumchukua Mwanajeshi mwenzao aliyekamwatwa na polisi hao kwa kosa la kuendesha pikipiki bila kuvaa kofia (Helmet).

Mashambuliazi hayo ya kurushiana risasi na kupigana ngumi na mateke yalitokea juzi jioni katika kituo hicho cha stendi ambapo Mganga Mfawidhi Hospitali ya Tarime alithibitisha kupokea majeruhi 12 na kati yao wawili ni askari wa JWTZ, Polisi saba na raia watatu.

Kamanda wa Polisi wa Tarime na Rorya, ACP Lazaro Mambosasa alisema Mwanajeshi huyo licha ya kukiuka taratibu za barabarani aliwatolea lugha za matusi polisi hao jambo lililowalazimu kumkamata kwa nguvu na wanajeshi wenzake kuingilia kati na kusababisha vurugu.

Alisema Wanajeshi watatu ambao hawakutajwa majina wameshikiliwa na polisi kwa kuvunja utaratibu wa usalama huku Mkuu wa Wilaya hiyo John Henjewele akilaani kitendo hicho cha kurushiana risasi za moto hewani na kusema ni cha utovu wa nidhamu na kilikwamisha shughuli za watu kwa muda sababu ya kuhofia usalama wao.

Unataka niwe nakusogezea kila stori inayonifikia zikiwemo pichaz, video’s na stori zenyewe? niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook cha kufanya ni kujiunga na mimi kwa kubonyeza

No comments:

Post a Comment