Monday 29 January 2018

ZIARA YA RC MNYETI WILAYANI SIMANJIRO

 Mkuu wa Mkoa Manyara Alexander Mnyeti (mwenye shati la maua) akiangalia mawe yaliyopo eneo la ujenzi wa nyumba ya walimu wa shule ya sekondari Emboreet Wilayani Simanjiro, ambayo ni pekee yenye kidato cha sita, inayojengwa na shirika la ECLAT Foundation na kuwasaidia wanafunzi wa eneo hilo hasa kutoka kwenye jamii ya kifugaji.
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti akizungumza na wananchi wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro alipotembelea kituo cha afya Mirerani na kubaini changamoto ya upungufu wa watumishi na uchache wa dawa.
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti akichoma zana haramu ikiwemo vyandarua, vyavu mlazo, mperampera na makokoro zinazotumika kwenye uvuvi haramu bwawa la Nyumba ya Mungu, kwenye Kijiji cha Magadini, Wilayani Simanjiro.
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti akiweka jiwe la msingi kwenye kiwanda cha madini ya Grafite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro, ambayo yatatumika kutengeneza kurunzi. 
Askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wanaojenga ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakichapia ukuta huo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa huo Alexander Mnyeti.  
 Wananchi wa Mji mdogo wa Orkesumet Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakitoa kero kwa Mkuu wa Mkoa huo Alexander Pastory Mnyeti. 


Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Pastory Mnyeti akizungumza na wananchi wa mji mdogo wa Orkesumet Wilayani Simanjiro.
 Wananchi wanne wa Kijiji cha Terrat Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakiwa kwenye gari la polisi baada ya Mkuu wa Mkoa huo Alexander Mnyeti, kuagiza wakamatwe kwa kudaiwa kusababisha migogoro ya Kijiji hicho
 Wananchi wa Kijiji cha Terrat Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakiwa na mabango, yanayoonyesha changamoto na kero walizonazo wakati wa kumpokea Mkuu wa Mkoa huo Alexander Mnyeti. 
 Wananchi wanne wa Kijiji cha Terrat Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakiwa kwenye gari la polisi baada ya Mkuu wa Mkoa huo Alexander Mnyeti, kuagiza wakamatwe kwa kudaiwa kusababisha migogoro ya Kijiji hicho
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Terrat Wilayani Simanjiro, ambapo aliwatangazia kuunda tume ya kuchunguza migogoro ya ardhi ya eneo hilo.
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti akizindua ujenzi wa nyumba ya walimu wa shule ya sekondari ya kidato cha sita ya Emboreet Wilayani Simanjiro, kwa kulima na jembe katika msingi wa nyumba hiyo, ambayo inajengwa kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikalli la ECTAL Foundation.  
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Terrat Wilayani Simanjiro, wakiwa na mabango, yanayoonyesha changamoto na kero walizonazo. 
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti akimsikiliza Mwenyekiti wa shirika lisilo la kiserikali la ECLAT Foundation alipokuwa akizungumza juu ya maendeleo ya chuo cha ufundi (Veta) kilichojengwa na shirika hilo.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti baada ya kupewa zawadi ya nguo ya jadi na wafugaji wa kata ya Naisinyai kwenye ziara yake Wilayani Simanjiro, kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo mhandisi Zephania Chaula na kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Jackson Leskar Sipitieck na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo Arnold Msuya.
Siku ya kwanza ya ziara ya siku saba ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti, kwenye Wilaya ya Simanjiro.

No comments:

Post a Comment