Tuesday 17 October 2017

FAINALI YA KOMBE LA USALAMA MANYARA KUFANYIKA OCTOBA 20

 Fainali ya soka ya mashindano ya Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Manyara, Usalama Cup inatarajiwa kufanya Octoba 22 mwaka huu. 

Msemaji wa mashindano hayo, Masudi Fupe akizungumzia michuano hiyo alisema mshindi wa mashindano hayo atapata kombe na sh1 milioni. 

Fupe alisema fainali hiyo itafanyika kwenye uwanja wa Kwaraa mjini Babati ambapo mshindi wa pili atapata zawadi ya 700,000. 

Alisema nusu fainali ya kwanza itawakutanisha timu ya Kariakoo ya Gidas kata ya Bonga dhidi ya City boys ya mjini Babati. 

Alisema nusu fainali ya pili itazikutanisha timu ya Veta SC ya Wang'warai dhidi ya Stend FC (chama la wana). 

"Pia mshindi wa tatu atapata zawadi ya sh450,000 mshindi wa nne atapata sh200,000 na kipa bora, mchezaji bora na timu yenye nidhamu atajipatia sh30,000 kila mmoja," alisema Fupe. 

Alisema timu 16 zilijitokeza kushiriki michuano hiyo kwa makundi manne na kila kundi lilitoa timu mbili zilizoingia robo fainali. 

Alisema lengo la mashindano hayo ni kutoa elimu kwa jamii juu ya kupunguza uhalifu, kupiga vita ujangili, kupinga mimba za utotoni na jamii kuwa karibu na polisi. 

"Siku ya fainali tunatarajia mgeni rasmi atakuwa mkuu wa mkoa wa Manyara, Dk Joel Bendera ambaye atakabidhi kombe kwa washindi na zawadi nyinginezo," alisema Fupe. 

No comments:

Post a Comment