Wednesday, 28 May 2014

KINANA AINGIA MANYARA







          Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana akipokewa na Mkuu wa Wilaya ya Hanang’ Mkoani Manyara, alipoanza ziara yake wilayani humo (kushoto) ni Katibu wa CCM Mkoani humo, Ndengasso Ndekubali na katikati ni Katibu Mwenezi wa CCM Mkoani humo, Fratey Massey na aliyekuwa Waziri Mkuu, Fredrick Sumaye.



Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye akisalimiana na  na Mkuu wa Wilaya ya Hanang’ Mkoani Manyara, ambapo yeye na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahaman Kinana, walipoanza ziara yao wilayani humo katikati ni Katibu Mwenezi wa CCM Mkoani humo, Fratey Massey

Monday, 26 May 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 26

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.




.

UCHAGUZI MARA GROUP

 Jamii ya Mara Group ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakiwa wamembeba Mwenyekiti wao, Philemon Oboro aliyechaguliwa jana kwa kupata kura 523 hivyo kuongoza jamii hiyo.
amii ya Mara Group ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakiwa wamembeba Makamu Mwenyekiti wao, Elija Ambonya aliyechaguliwa jana kwa kupata kura 363 hivyo kuongoza jamii hiyo.


Jamii ya Mara Group ya Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, imemchagua Philemon Oboro, kuwa Mwenyekiti wake kwa kipindi cha miaka mitatu baada ya kuwaangusha wapinzani wake watatu.
 
Akitangaza matokeo hayo jana, Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi huo Samwel Ombeng alisema Oboro alipata kura 523, Philipo Mtanda Onyando kura 60, Allan Gichana kura 33 na Jackson Onyango Mutaban kura nane.
 
Ombeng alisema Elija Ambonya alichaguliwa kuwa Mwenyekiti Msaidizi kwa kupata kura 363 na kumshinda Thobias Magati aliyepata kura 305 na Stephen Odoya, alichaguliwa kuwa Mweka hazina, baada ya kukosa mpinzani.
 
Naye, katibu wa tume hiyo Gerald Orinya (Team Coach) alisema Elija Ambonya alichaguliwa kuwa Katibu wa Mara Group kwa kupata kura 363 na kuwashinda Adam Wambura kura 117, Msafiri Marwa kura 130 na Omenda Odero kura 84.
 
Orinya alisema George Okwaro alishinda nafasi ya Katibu msaidizi kwa kupata kura 378 na kumshinda Samwel Orafa aliyepata kura 221 na Asubuhi Kibaso alishinda nafasi ya Kamanda wa Mara Group, baada ya kupita bila kupingwa.
 
Katibu wa Utegi kaskazini, Atanas Ongati (Power Tiler) alisema lengo la Mara Group ni kusaidiana kwenye shida na raha na kuhakikisha watu wote wanaofariki wakiwa Mirerani wanasafirishwa na kwenda kuzikwa nyumbani kwao mkoani Mara.
 
Akizungumza baada ya kuchaguliwa, Oboro alisema atawaongoza ipasavyo wana kikundi hao bila ubaguzi na dhamira yake ni kuwaunganisha pamoja kwa kutojali waliompigia kura au wasiompigia kwani wote ni wamoja.
 
Naye, Mwenyekiti msaidizi Ambonya alisema kupitia ushirikiano walionao watahakikisha Mara Group inazidi kuimarika na kusaidiana na jamii yote ya mji mdogo wa Mirerani bila kujali tofauti, kwani ushirikiano ndiyo nguzo ya umoja.
 


Thursday, 22 May 2014

WAJUMBE WA HALMASHAURI YA CCM BABATI MJINI

Diwani wa kata ya Bonga Mjini Babati Mkoani Manyara, Pasian Siay akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri ya CCM ya wilaya ya Babati.

Katibu wa CCM wa Mkoa wa Manyara, Ndengasso Ndekubali akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri ya wilaya ya Babati mjini.

Wajumbe wa Halmashauri ya CCM Babati mjini Mkoani Manyara wakifuatilia kikao cha Halmashauri ya wilaya hiyo.

ZIMAMOTO

Mwanafunzi wa shule ya msingi Babati Mkoani Manyara wakipatiwa elimu ya zimamoto na uokoaji wakati askari wa jeshi la zimamoto na uokoaji Manyara walipokuwa wanatoa elimu ya zimamoto shuleni hapo

Wanafunzi wa shule ya msingi Babati Mkoani Manyara wakipatiwa elimu ya zimamoto na uokoaji, wakati askari wa jeshi la zimamoto na uokoaji Manyara walipokuwa wanatoa elimu ya zimamoto shuleni hapo

WACHIMBAJI MADINI TANZANITE

Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara, Christopher Ole Sendeka akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani

Diwani wa Kata ya Endiamtu Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini 

Wanachama wa CCM na wachimbaji wadogo wa madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakimpokea Mbunge wa Jimbo hilo Christopher Ole Sendeka

MJASIRIAMALI

Mjasiriamali Teddy Jacob akiwa saluni kwake Kiwi Beauty iliyopo Mji mdogo wa Haydom Wilayani Mbulu Mkoani Manyara.

WAUGUZI HANANG

Wauguzi wa Wilaya ya Hanang' Mkoani Manyara wakiandamana wakati wa kuadhimisha siku ya wauguzi duniani ambapo wao walichelewa kufanya Mei 12 kutokana na kuwa na wagonjwa wengi 
Mkuu wa Wilaya ya Hanang Christina Mndeme akizungumza na waguzi wa wilaya hiyo 

Mkuu wa Wilaya ya Hanang Christina Mndeme akizungumza na waguzi wa wilaya hiyo 

Wednesday, 21 May 2014

TUNAPASUA KUNI



Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Measkroni Wilayani Hanang Mkoani Manyara, wakipasua kuni za kupikia chakula shuleni hapo