Tuesday, 20 October 2015

KAMPENI YA CCM KATA YA ENDIAMTU



Wakereketwa, wapenzi na wananchama wa CCM Kata ya Endiamtu Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakiwa kwenye kampeni ya kumnadi mgombea udiwani Lucas Chimba Zacharia

Sunday, 11 October 2015

Thursday, 1 October 2015

MWENGE WA UHURU MKOANI MANYARA



Mara baada ya kuhitimisha mbio za mwenge wa uhuru tulipoukimbiza Mkoani Manyara



Wakimbiza mwenge kitaifa Karim Haruna (kushoto) na Arnold Litimba wakikagua zao la kitunguu kwenye kijiji cha Gunge Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, mara baada ya mwenge wa uhuru kutembelea wilayani humo



Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, Juma Khatibu Chum akizindua mradi wa barabara ya Bassodesh-Mulbadaw jana Wilayani Hanang' Mkoani Manyara.

Wednesday, 23 September 2015

KAMANDA UVCCM SIMANJIRO DANIEL OLE MATERI

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana akimkabidhi cheti na kumpongeza Mkurugenzi wa Grace Land Hotel Daniel Ole Materi ambaye ni Kamanda wa UVCCM Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, katikati ni Mkuu wa wilaya hiyo Mahmoud Hashim Kambona na Katibu wa CCM mkoani humo Ndeng'aso Ndekubali.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana akimkabidhi ngao Mkurugenzi wa Grace Land hotel Daniel Ole Materi na kumsimika kuwa Kamanda wa UVCCM Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara.
Kamanda wa vijana wa UVCCM Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Daniel Ole Materi akiwapungia mkono wakazi wa Mji mdogo wa Mirerani, baada ya kusimikwa na Ktibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana.

LUCAS ZACHARIA

Katibu Uchumi na Fedha wa CCM Mkoani Manyara, Lucas Chimbason Zacharia akijinadi mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Omary Kinana, kwa wakazi wa Mji mdogo wa Mirerani wakati akiomba kuchaguliwa kuwa diwani wa Kata ya Endiamtu.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahaman Kinana akimsikiliza Katibu Uchumi na Fedha wa CCM Mkoa wa Manyara, Lucas Zacharia wakati akiomba kura ili achaguliwe tena kuwa Diwani wa Kata ya Endiamtu.
Mgombea udiwani wa Kata ya Endiamtu Wilayani Simanjiro Lucas Chimbason Zacharia ambaye pia ni Katibu Uchumi na Fedha wa CCM mkoani Manyara, akiwaomba kura wakazi wa kata hiyo.