Wednesday, 23 September 2015

MAGUFULI BUKOBA

 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John  Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa Gymkhana mjini Bukoba tayari kuhutubia wakazi wa Manispaa ya Bukoba.

Umati wa wakazi wa manispaa ya Bukoba wakiwa wamefurika katika viwanja vya Gymkhana kumsikiliza mgombea Urais kupitia CCM Dk. John Magufuli .

MTWARA MOJA

LOWASSA AWASHUKURU WANANCHI WA MASASI KWA MAPOKEZI MAKUBWA ALIYOYAPATIA

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwasili kwenye Uwanja wa Boma, Mjini Masasi Mkoani Mtwara, kulikifanyika Mkutano wake wa Kampeni za kuomba ridhaa ya wananchi kugombea nafasi, uliofanyika leo Septemba 22, 2015.


Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara, waliofikia kusikiliza sera zake katika Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Boma, leo Septemba 22, 2015. Ambapo amewashukuru wananchi wa Mji wa Masasi kwa mapokezi makubwa waliyompatia.
Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye akizungumza machache na wananchi wa Jimbo la Masasi Mjini, Mkoani Mtwara waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Boma, leo Septemba 22, 2015.CHANZO OTHMAN MICHUZI
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwapungia mkono wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara, muda mfupi baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Boma, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni, leo Septemba 22, 2015.
Uwanja wa Boma mjini Masasi, palikuwa hapatishi pale Mgombea Urais alipowasili uwanjani hapo.

Mgombea wa Ubunge anaekubalika na wananchi wa Masasi kupitia Mwamvuli wa Chama cha Wananchi CUF, Ismail Makombe (Maarufu kwa Jina la Kundambada), akizungumza machache na wananchi hao waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Boma, leo Septemba 22, 2015.
Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa kupitia Chama cha NLD, Dkt. Emmanuel Makaidi akiwa ameambatana na Mkewe, wakiwasalimia wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara leo Septemba 22, 2015.
Chademaaaaaa.........
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akipokea karatasi ya Shairi kutoka kwa Msoma Mashairi, Mohamed Ally (kushoto) mara baada ya kughani Shairi lake.

Magambo yenye jumbe mbali mbali.
Sehemu ya Wananchi wa Mji wa Masasi, Mkoani Mtwara wakiwa katika Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Boma, leo Septemba 22, 2015.

Thursday, 17 September 2015

MAFURIKO GEITA

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akihutubia Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya Zamani ya Chato, Wilayani Chato, Mkoani Geita  Septemba 16, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akimnaji Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chato, Dkt. Benedicto Lukanima, katika Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya Zamani ya Chato, Wilayani Chato, Mkoani Geita  Septemba 16, 2015.
Mh. Tundu Lissu akiwasalimia wananchi wa Jimbo la Chato, Mkoani Geita  Septemba 16, 2015.
Waziri Mkuu wa zamani, Mh. Fredrick Sumaye, akihutubia Mkutano wa hadhara wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Stendi ya Zamani ya Chato, Wilayani Chato, Mkoani Geita  Septemba 16, 2015.




















Sunday, 13 September 2015

GEKUL AZINDUA KAMPENI YAKE JIMBO LA BABATI MJINI



Mgombea ubunge  Jimbo la Babati Mjini kwa tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Pauline Gekul ataboresha huduma za jamii na kuwatetea wananchi katika vyombo vya maamuzi, pindi akichaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.

Akizungumza mjini Babati kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho, Gekul alisema endapo atapewa ridhaa na wananchi atadhibiti wizi uliokithiri kwenye halmashauri na kuboresha huduma katika sekta zote.
Alisema akipewa ridhaa hiyo atasimimia ulipwaji wa madai ya watumishi kwa wakati na hasa walimu, madaktari, wauguzi na polisi na kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifundishia katika shule za msingi na sekondari, uanzishwaji wa madarasa ya awali katika shule za msingi na ujenzi wa mabweni katika shule za kata.

“Nitajenga  wodi mpya za wazazi hospitali ya Mrara na kupigania vifaa tiba katika hospitali na zahanati, kuanzishwa na kuboreshwa kwa huduma za masoko madogo madogo na kuwaunganisha vijana na  fursa za ajira na kujiajiri wenyewe,” alisema Gekul.

Alisema ataendelea kupigania vifaa tiba vipatikane katika hospitali, vituo vya afya na zahanati, kuanzisha na kuboresha huduma za masoko madogo madogo katika mitaa yetu, kuwaunganisha vijana na fursa za ajira na kujiajiri wenyewe.

Pia, mgombea huyo aliibua ufisadi wa kutisha  unaofanywa katika halmashauri hiyo huku akishirikiana na wafuasi wake kusoma kitabu cha bajeti na kuonyesha namna ambavyo madiwani walivyotumia fedha za walipakodi.

 “Ninaomba mnitoe kuwa msaidizi mnikabidhi jimbo ili niweze kuwatumikia kikamilifu kama nilikua nafanya nikiwa viti maalum na sikuwa na fungu nikipewa ndiyo nitashindwa jamani naomba mniamini wana Babati,” alisema  Gekul.

Nao, baadhi ya wananchi wa eneo hilo, Restituta Martin, Mussa Hassan na Michael Boay walisema huu ni wakati kwa wananchi wa mji huo kumchagua Gekul ambaye amekuwa akiwatetea wananchi wanyonge hasa migogoro yao.