Mgombea Uenyekiti wa Kitongoji cha Tunduru, Mji
mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Christopher Chengula akinadi
sera za Chadema kwenye mkutano wa kampeni.
Wakazi wa Kitongoji cha Tunduru, Mji mdogo wa
Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakimsikiliza mgombea Uenyekiti Christopher
Chengula akinadi sera za chama hicho kwenye mkutano wa kampeni.
Katibu Mwenezi wa Chadema Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Ambrose Ndege akizungumza na wakazi wa Kitongoji cha Tunduru, wakati akinadi sera za chama hicho kwenye mkutano wa kampeni.
Mgombea Uenyekiti wa Kitongoji cha Kazamoyo Juu David Kyara, akizungumza na wakazi wa Kitongoji cha Tunduru, Mji mdogo wa
Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kwenye mkutano wa kampeni wa Chadema.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Elaston Mbwilo ( wapili kulia) akiwakabidhi Diwani
wa Kata ya Ganana, Wilayani Hanang’ Zacharia Tarmo na Diwani wa viti maalum
Juliana Songai, moja kati ya mifuko 100 ya saruji yenye thamani ya sh1.7
milioni iliyotolewa na wakuu wa idara wa halmashauri ya wilaya hiyo, kulia ni
Mkuu wa wilaya hiyo Christina Mndeme na katikati ni Mkurugenzi mtendaji wa
halmashauri hiyo Filex Paul Mabula.