Thursday, 14 June 2012

PUNDAMILIA

Punda milia wa hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro

TWIGA WA NGORONGORO

Twiga wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro

Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Margareth Zziwa akizungumza mjini Arusha baada ya kuchaguliwa hivi karibuni

MAGUFULI

Jengo la Lusona House likiwa limevunjwa na wamiliki wake kwa amiri ya waziri wa Ujenzi John Magufuli

Sunday, 27 May 2012

KAMANDA

Kamanda

KAMANDA NASARI


Kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa kunijalia kuwa mbunge kwani nilikuwa na maono ya tangu siku nyingi kuwa mbunge wa Jimbo hili,pia nakishukuru chama changu cha CHADEMA kwa kunipa ridhaa ya kugombea na pia kwa nafasi ya pekee kwa kweli nawashukuru sana watu wa Arumeru Mashariki ambao hawakujali umri wangu,hawakujali uwezo wangu kifedha,hawakujali historia ya familia yangu katika siasa,hawakujali kila mapungufu ambayo nilikuwa nayo,lakini wakaamua kunichagua….Najua walikuja wengi na fedha nyingi,najua walikuja wengi na majina makubwa,najua walikuja wengi na kila aina ya mbwembwe,walikuja wengi na bendi nyingi za muziki,walikuja wengi wakahonga sana,walikuja wengi wakanitukana sana,walikuja wengi wakanisema sana…Lakini hatimaye sauti ya wengi imekuwa sauti ya Mungu na lile alilolipanga Mwenyezi Mungu limekwenda kutimilika,tangu mwanzo nilisema tunaanza na Mungu tunamaliza na Mungu….Walipoambiwa kuwa mimi ni mdogo kiumri wakasema siendi Bungeni kupeleka mvi au kupeleka miaka na tena wakasema wanahitaji dogo janja na siyo kubwa jinga…..Walipoambiwa kuwa mimi sijaoa wakasema siendi Bungeni kusuluhisha ndoa,walipoambiwa sina kitambi wakasema siendi kucheza mieleka Bungeni na walipoambiwa mimi ni masikini wakasema tunamuhitaji masikini mwenzetu…Narudia tena kama nilivyosema mwanzo tumeanza na Mungu na tunamaliza na Mungu….Kamanda Joshua Nassari mara baada ya kutangazwa kuwa Mbunge Mteule Jimbo la Arumeru Mashariki Aprili 2 mwaka huu.

Friday, 25 May 2012

MAKAMU WA RAIS

Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilal katika mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika nchini Botswana

DC SIMANJIRO

Mkuu wa wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,Peter Toima akihojiwa na waandishi wa habari mara baada ya kula kiapo

Thursday, 10 May 2012

KAMANDA

Kwenye siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani nikiwa na Kamanda wa polisi mkoani Manyara Kamishna Msaidizi Liberatus Materu Sabas

PICHA

Mti wa pesa eneo la Chandama wilaya ya Chema mkoani Dodoma